Arc Hoteli

Morogoro, Tanzania

 

 Wapendwa wageni wetu,

 Karibuni Arc, hoteli iliyopo Morogoro , Tanzania .

 Arc hoteli imefunguliwa hivi karibuni, ni hoteli ya kisasa iliyo katika viwango vya kimataifa. Ipo pembezoni mwa mji wa Morogoro, 
 kama kilomita 2 toka   katikati ya mji, kandokando mwa barabara kuu ya Dar es Salaam kuelekea Dodoma au Zambia.

  Arc hoteli inatoa huduma nzuri ya vyumba vya kulala kwa mtu mmoja mmoja, wawili wawili au zaidi.  
  Vyumba vyake  vinatazama 
mandhari nzuri ya milima ya Uluguru.

 Mgahawa wa Arc hoteli unaoitwa “Mikumi” hutoa huduma ya vyakula mbalimbali, vinavyotolewa ama ndani au nje kwenye eneo
 la wazi lenye hewa safi na upepo mzuri utokao milimani. Huduma katika mgahawa huu ni pamoja na kifungua kinywa, chakula
 cha mchana na jioni/usiku. Vyakula hivi ni vya mapishi ya
Kiafrika, Kihindi, Kichina, Kimataifa,
 
na vinginevyo vya kimataifa ambavyo hutayarishwa na wapishi wataalamu katika jiko lenye vifaa mbalimbali vya kisasa.

  Sisi kutoa viwango maalum kwa ajili ya vyama na karamu.

 Aidha, Arc hoteli ina ukumbi wa mikutano unaoitwa “Udzungwa” wenye uwezo wa kupokea hadi watu 45 kwa ajili ya mikutano,
 semina au warsha.

 Huduma zitolewazo katika eneo lililowazi ni pamoja na huduma za baa iitwayo “Wami-Mbiki”; hapo ni mahali utakapofurahia 
 vinywaji mbalimbali baridi au moto mara baada ya vipindi vya mkutano. 

                                                    Information about the Arc Hotel (pdf document)     Visit to the Arc Hotel   
 
Write a review on


   KUPATA  NAFASI  MAWASILIANO  MALAZI   MAHALI ILIPO   PICHA   UTALII: WA KIUTAMADUNI ENGLISH  

PICHA MBALIMBALI 
 

TAARIFA MUHIMU

hotelentrance2

Uluguru mountains room2 Arc Hotel

Arc Hotel Arc Hotel Arc Hotel
B
ofya katika picha, ili uikuze - Photo Gallery


 Jinsi Ya Kutufikia

 Arc Hoteli ipo pembezoni mwa mji wa Morogoro, kama kilomita 2 toka katikati ya mji,
 kandokando ya barabara kuu ya Dar es Salaam kuelekea Dodoma au Zambia.

 Ipo mahali panapopendeza chini ya milima ya Tao la Mashariki na hasa karibu kabisa
 na milima ya Uluguru, Hoteli hii huonekana kwa urahisi upande wa kushoto katika
 barabara kuu ukitokea Dar es Salaam unapokaribia mji wa Morogoro kama
 inavyoonyeshwa katika ramani hapa chini.

Arc Hotel map
Bofya katika Ramani ili uikuze

 View slide show:



_______________________
 Visit us at:

                 

 

     Muda wa kutoka:  Saa 5 asubuhi
  Muda wa kuingia:  Saa 6 mchana
CREDIT CARDS ACCEPTED
Visa Visa
Master Card Master Card
Eurocard Eurocard

HUDUMA KWA UJUMLA

Baa
Gari la kukodi
Baa ya kokteli(mchapalo)
Huduma za mikutano
Kifungua kinywa aina ya kimagharibi
Ukumbi wa chakula
Udobi
Huduma za Intaneti
Maegesho salama ya magari
Mgahawa
Huduma za vyumbani
Vyumba vyenye luninga
Huduma ya kuamshwa
 
HUDUMA ZA VYUMBANI
Kiyoyozi
Huduma za dobi
Mahali binafsi pa kuogea
Simu
Luninga
 

 SERA YA WATOTO
 Arc Hoteli inazikaribisha pia familia zenye 
 watoto. 
 Hoteli inao uwanja wenye michezo mizuri kwa
 watoto.

 

 
Lugha za mawasiliano
 
Kiingereza
 Kiswahili

 HUDUMA ZITOLEWAZO
 Burudani ya michezo kama vile mpiro wa miguu, muziki,
 sinema, "dokumentari" n.k. kupitia Luninga kubwa, DSTV,
 na sehemu maalumu ya kuoneshea burudani hizo.

 Gharama za Huduma
 Chumba mtu mmoja: TZs 70,000.00
 Chumba cha watu wawili
: TZs 90,000.00
 Apartment - suite: TZs 180,000.00
 T
Zs 20,000.00 zinaongezeka kwa kila mtu mmoja
 anayeongezeka chumbani.
 Gharama hizi zinajumuisha mlo kamili wa asubuhi yaani
 kifungua kinywa.

 
 KUPATA NAFASI
 Tutumie ujumbe wa maulizo 
 k
atika mtandao kupitia booking form 
 au
tuma barua pepe kwenda:
 
booking@archotel-tz.com

 Kwa Mawasiliano tuandikie:
 
D. Matovelo
 Arc Hotel
 P.O. Box 3112
 Morogoro, Tanzania

 Unaweza kupiga simu kama ifuatavyo:

Simu uwapo nchini: 023 2600250
Faksi uwapo nchini: 023 2600240
Simu uwapo nje ya nchi: +255 23 2600250
Faksi uwapo nje ya nchi: +255 23 2600240
Simu ya mkonomi: 0769 600240
          Simu ya mkononi uwapo nje: +255 769 600240
                                               Email: info@archotel-tz.com